Mwanamume ambaye alidanganya kuwa kiwete akamatwa na Dhahabu nchini Bangladesh.

 

Mwanamume ambaye alidanganya kuwa kiwete aliyekuwa akitumia kiti cha magurudumu na ambaye alikuwa amefunga dhahabu ya kilo 25 kwenye mapaja yake, amekamatwa kwenye uwanja wa ndege nchini Bangladesh.

Maafisa wa forodha walishuku wakati waligundua kuwa Jamil Akhter, alikuwa amesafiri mara 13 mwaka huu.
Dhahabu hiyo ya gharama ya dola milioni 1.5 ndiyo kubwa zaidi kukamatwa mwaka huu wakati Bangadesh ilibuka kuwa kituo cha kupitisha dhahabu kwenda nchini India.
Kupanda kwa kodi kwa dhahabu nchini India iliyo mnunuzi mkubwa zaidi wa dhahabu duniani kumechangia kuongezeka visa vya uiafarishaji wa dhahabu kwa njia haramu.

No comments:

Post a Comment